KAMA UMEWAHI KUSIKIA NENO "NGEKEWA" BASI LIMETOKANA NA MNYAMA HUYU - MUKAMAFUNNY BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, March 5, 2018

KAMA UMEWAHI KUSIKIA NENO "NGEKEWA" BASI LIMETOKANA NA MNYAMA HUYU

1.Mnyama anayefahamika kwa jina la kigeni Capybara ambapo kwa kiswahili huitwa Ngekewa ni mnyama mwenye ukubwa wa sentimita 134 na uzito unaokadiliwa kuwa kilo 66 anapokuwa mkubwa na mnyama huyu asili yake ni nchi ya America ya kusini.       

2. Ni mnyama ambaye anapenda kukaa karibu na maji na anapojisi hatari hulazimika kukimbilia ndani ya maji na ana ujuzi mkubwa wa kuogelea.

3. Akiwa ndani ya maji anaweza kutumia dakika tano bila kuibuka ambapo hubana pumzi ndani ya maji anapokwepa hatari ya kushambuliwa na adui yake.

4. Huyu Ngekewa ndio mnyama anayependwa na viumbe vingi vya porini na majumbani.
Wanyama kama mamba, chatu, nyani, paka, kobe na hata ndege wa aina mbali mbali hupenda kukaa karibu naye na kufurahia maisha hivyo mnyama huyu huhesabika kama kiumbe chenye bahati ya kupendwa na viumbe wengine ukiondoa maadui zake.

 5. Kwenye kamusi ya lugha ya kiswahili neno Ngekewa mbali na kumzungumza huyu mnyama pia limetafsiliwa kama bahati au yenye bahati na ndio maana hata mtaani mtu mwenye bahati huambiwa ana ngekewa.
Asili ya maana ya neno ngekewa ipo katika kupendwa kwa huyu mnyama na viumbe mbali mbali hata vile vya hatari.

2 comments:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages