Mashindano ya KIA marathon yamefanyika jana Jumapili Novemba 19 katika uwanja wa kimataifa wa ndege KIA uliopo mkoani kilimanjaro na kushirikisha zaidi ya nchi 40 duniani kote.
| Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa KADCO akizungumza na Mukama Funny Media |
Hayo yamethibitisha na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa KADCO Bw. Christopher Mkoma ambaye ndiye msimamizi wa uwanja na kusema kuwa wameandaa mashindano hayo kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika nchi yetu ili kuongeza pato la taifa kupitia utalii wa ndani.
Hata hivyo aliongeza na kusema kuwa kupitia mashindano hayo yamekua hamasa kubwa kwa wanariadha wa hapa nchini kwani wameweza kuchuana na wanariadha kutoka nchi mbalimbali ikiwemo kenya,uganda, afrika kusini na sudani.
Naye Meneja masoko wa KADCO Bi.Christina Mwakatobe ameyataka makampuni na Taasisi mbalimbali kujitokeza kudhamini mashindano hayo kwani wataweza kutangaza biashara zao na kuweza kuchangia kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii vilivyopo hapa nchini.
| Meneja Masoko wa KADCO |
Kwa upande wake Rais wa riadha nchini Mh. Antony Mtaka ameshukuru washiriki wote kutoka mataifa mbalimbali na kuwata watanzania kushriki zaidi na kushinda ili kuitangaza nchi
| Baadhi ya Washiriki Wa mbio za Km 21 Wakiwa na Medani zao baada kumaliza Mbio |
| Rais wa Riadha Tanzania Bw. Antony Mtaka Akizungumza na waadishi wa habari |

No comments:
Post a Comment