WAPALESTINA WAPINGA TANGAZO LA TRUMP KWA KUZIMA TAA ZA KRISMASI MJINI BETHLEHEM - MUKAMAFUNNY BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 7, 2017

WAPALESTINA WAPINGA TANGAZO LA TRUMP KWA KUZIMA TAA ZA KRISMASI MJINI BETHLEHEM

Wapalestina wamezima taa za krismasi kwenye mji mtakatifu wa Bethlehem alikozaliwa Bwana Yesu, kupinga hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kuutambua mji wa Yerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Afisa Habari wa Manispaa ya Bethelehem, Fady Ghattas amesema Mti wa Krismasi ulioko kwenye kanisa la Bethlehem ambako wakristo huamini Bwana Yesu alizaliwa, ulizimwa taa zake kwa amri ya Meya wa Manispaa hiyo.

Miji mingine iliyozimwa taa ni Ramallah ulio karibu na mahali alipozikwa kiongozi wa zamani wa Palestina Yasser Arafat.

Waarabu na waislamu katika nchi za Mashariki ya kati wamepinga hatua ya Trump ya kutangaza kutambua Yerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages