Jumapili ya leo Januari 21, 2018 Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan amewatupia ujumbe mzito wananawake wote wa Tanzania huku akiwasihi kuungana ili kuwa na sauti moja bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Mama Samia ameyasema hayo kupitia akaunti yake ya Instagram ambapo amewasisitiza wanawake wote kuungana na kuwa na sauti moja katika kulinda na kutetea haki zao huku wakiweka pembeni itikadi zao za kisiasa.
"Wanawake ni lazima tuwe na kimoja na sauti moja katika kulinda na kutetea haki zetu bila kujali itikadi za kisiasa" aliandika makamu wa Rais mama Samia Suluhu.
No comments:
Post a Comment