MFAHAMU ZAIDI MNYAMA AITWAYE PIMBI....ANAWEZA KULA VITU VYENYE SUMU NA AKAENDELEA KUISHI. BOFYA HAPA CHINI UELIMIKE KWA MAKALA HII TAMU - MUKAMAFUNNY BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 14, 2018

MFAHAMU ZAIDI MNYAMA AITWAYE PIMBI....ANAWEZA KULA VITU VYENYE SUMU NA AKAENDELEA KUISHI. BOFYA HAPA CHINI UELIMIKE KWA MAKALA HII TAMU

 ‘PIMBI’ kwa lugha ya kigeni wanamwita ‘HYRAX’.



UTANGULIZI


Pimbi ni jamii ya wanyama wenye maumbile madogo na vimo vifupi sana ambao wanapatikana maeneo mbalimbali hasa barani Afrika. Ni jamii moja tu ya pimbi ambayo inapatikana nje ya bara la Afrika na maeneo ya ghuba za Arabuni kutokea nchi ya Lebanon hadi maeneo ya Saudi Arabia. Wanyama hawa kutokana na maumbile yao madogo huwa ni vigumu sana kuwaona na bila kuwa makini unaweza zunguka hifadhini hata mwezi mzima bila kuwaona kwani huwa wana tabia ya kujificha sana kwenye mazingira wanayoishi. Hivyo unapokuwa unatalii katika hifadhi za wanyamapori unapaswa kuwa makini zaidi katika uchunguzi hasa maeneo yenye miamba 

Kuna jamii mbali mbali za Pimbi ambazo kwa utafiti inasemekana kuna jamii tatu za wanyama hawa. Jamii hizi ni kama ifuatavyo mbili kati ya tatu hujulikana kama Pimbi wa kwenye miamba na moja ni Pimbi wa kwenye miti. Jamii zote hizi hufanana sana kwa muonekano na ukubwa wa mwili.

PIMBI WA KWENYE MIAMBA (ROCK HYRAX).

SIFA NA TABIA ZA PIMBI WA KWENYE MIAMBA

Pimbi ni wanyama wanaofanana au kuonekana kama sungura kwani wana miguu mifupi, mikia mifupi sana ( sawa na hawana mikia kabisa) na masikio ya duara. Sifa hizi zimepelekea wanyama hawa kupewa jina la Sungura wa kwenye miamba kwani wana fanana sana na sungura.

Dume na jike huwa wana fanana sana kwa ukubwa na huwa ni vigumu sana kwa mbali kuweza kuwatofautisha kati ya jike na dume kutokana na kufanana kwao. Hivyo kuweza kuwatofautisha kati ya jike na dume lazima uweze kuwashika au kuwa karibu zaidi.

Pimbi ukiwachunguza vizuri katika nyayo za miguu na viganjani wana alama kama vitufe vyenye matezi mengi sana ya jasho. Matezi na alama hizi za vitufe huwasaidia wanyama hawa kuweza kukimbia na kushikilia kwenye miamba vizuri wakati wana kimbia.

Kwa ujumla ukimchunguza vizuri utagudua ana alama nyeupe kwa juu ya macho na sehemu ya juu anakuwa na rangi ya weupe wuepe inayoelekea kuwa kama manjao. Rangi hii inaweza kuonekana kwa baadhi ya jamii nyingine za pimbi japo huwa huwa haiwezekani kwa jamii moja kuzaliana na jamii nyingine.

Wana manyoa marefu yaliyo enea mwili mzima na yenye rangi ya manjano au kijivu ifananyo na kahawia. Pimbi pia wana matezi ya juu ambayo yamezungukwa na rangi kama ya utadu wa maziwa au manjano na wakati mwingine kahawia iliyokoza sana au mzunguko wa manyoa meusi ambayo husimama kipindi pimbi anapokuwa na hasira.

Mbali na kuwa ni jamii ya wanyama wenye damu moto, lakini pimbi ni wanyama ambao wana uwezo mdogo sana wa kurekebisha jotoridi la mwili na kiasi kidogo sana cha mmeng’enyo wa chakula ukilinganisha za ukubwa wa miili yao. Jotoridi katika miili yao hurekebisha kwa njia za kukusanyika pamoja, kukaa muda mrefu bila kufanya shughuli yoyote au wakati mwingine kwa kujitutumua. Hivyo kitu cha kwanza kukifanya asubuhi wanapo amka huwa wana lala kwenye miamba ili kupata joto.

Pimbi hawa huishi kwenye kundi ambalo huwa na kiongozi ambae ni dume mtawala. Hii ni tofauti na pimbi wa kwenye miti ambao huishi kwa kujitenga japo ni mara chache sana kuona kundi la pimbi wawili hadi watatu katika jamii hii ya pimbi wa kwenye miti.

Pimbi wa kwenye miamba huwa wana uwezo wa kuona zaidi majira ya asubuhi na mchana tofauti na pimbi wa kwenye miti ambao wao wana uwezo wa kuona zaidi majira ya usiku.

Pimbi hutumia sehemu moja kwa kukojolea na haja kubwa. Pimbi wote ndani ya kundi huwa na desturi ya kuchagua sehemu maalumu ya kukojoa na haja kubwa na si kufanya hivyo kila mahali.

Huwasiliana kwa njia ya sauti za miguno, mngurumo au kama filimbi na wakati huu kundi moja huweza kuliitikia kundi lingine popote walipo.

UREFU, KIMO NA UZITO

Urefu= Pimbi hawa wa kwenye miamba huwa na urefu wa takribani sentimeta sm 30 – sm 56

Kimo=hufikia kim cha sentimeta sm 23 – sm 30

Uzito= Pimbi hawa huwa na uzito wa hadi kilogramu kg 3 – kg 5

MAZINGIRA

Pimbi wa kwenye miamba wameenea sana barani Afrika. Hupendelea kuishi kwenye miamba sana. Kwa hapa kwetu Afrika mashariki pimbi hawa wanapatikana maeneo yenye muinuko wa futi takribani 14,000 kutoka usawa wa bahari.

Ukitembelea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha utaweza kuwaona wanyama hawa vizuri sana kutokana na baadhi ya maeneo ya hifadhi hii kuwa na miamba mingi sana.

CHAKULA

Pimbi hawa ni miongoni mwa jamii ya wanyama walao majani, hivyo kwa ujumla tunasema chakula kikubwa cha wanyama hawa ni kile chenye asili ya mimea Japo kuna wakati mwingine wanyama hawa hula wadudu na baadhi ya viumbe jamii ya reptilian kama mijusi.

Huwa wanapenda kula majira ya asubuhi kabla jua halijawa kali zaidi na desturi yao katika ulaji huwa wanakula kwa kutengeneza duara ili kuweza kuona pande zote kwa ajili ya kuwaepuka maadui zao. Na maranyini pimbi hawa huwa wanakula maeneo ambayo yapo karibu sana na makazi yao kwani inakuwa ni rahisi kukimbia na kujificha ndani ya miamba.

Vyakula ambavyo wanapendelea sana wanyama hawa ni majani, matunda, wadudu, mijusi na wakati mwingine mayai ya ndege. Wana uwezo wa kuishi muda mrefu sana bila kunywa maji kwani wanapata maji yakutosha sana kutoka kwenye vyakula wanavyo kula.

KUZALIANA

Pimbi hawa huishi kwa makundi na makundi zaidi ya moja huweza kuishi kwenye eneo moja. Pamoja na kundi zaidi ya moja kuishi kwenye eneo moja, bado huwa kuna utawala kwa madume. Kila dume huwa na mipaka yake na anaweza kumiliki hadi majike ishirini kwa wakati mmoja.

Jike huwa anazaa mara moja tu kwa mwaka na maranyingi wanyama hawa hupandana majira ya joto kisha watoto kuzaliwa majira ya kipupwe. Mara baada ya kupandana jike hukaa na mimba kwa muda wa miezi saba hadi saba na nusu. Hii inamfanya mnyama huyu kuwa ndo mnyama mwenye umbo dogo pekee ambae anakaa na mimba kwa muda mrefu kuliko wanyama wote wadogo duniani.

Katika familia moja majike wote wenye mimba wanapoanza kuzaa basi watazaa na kumaliza wote ndani ya wiki tatu tu na kwa jamii hii ya pimbi jike huzaa watoto kuanzia 1 – 4. Watoto huzaliwa wakiwa wamekamilika na huweza kukimbia na kuruka mara tu baada ya saa moja tangu kuzaliwa. Watoto huwa chini ya uangalizi kwa takribani miezi mitano na wote kwa pamoja wakike na kiume huwa tayari kwa kuzaa wafikishapo miezi 16 – 17.

Wafikishapo umri wa miezi 16 hadi 17 watoto wa kike hujiunga na kundi la kina mama huku watoto wa kiume huanza kujiandaa kuondoka ndani ya kundi hilo kutokana na kufukuzwa na madume na hapo ni kabla hawajafikisha miaka mitatu ( yaani takribani miezi 30), japo wengi wao huondoka wakiwa na miezi 16 – 24. Maisha ya pimbi kutokana na tafiti mbali mbali huwa ni miaka 8 – 12.

UHIFADHI

Mpaka sasa pimbi wa miamba hawajawa kwenye mjadala wa kiuhifadhi kutokana na shirika la umoja wa mataifa linaloshughulika na uhifadhi wa maumbile asili (International Union for Conservation of Nature- IUCN). Hii ni kutokana na kwamba wanyama hawa bado wametawanyika au kupatikana kwa wingi katika maeneo tengefu ya uhifadhi wa wanyamapori. Japo jambo la kushtusha ni kwamba jamii ya pimbi wa miti wamekuwa wakiwindwa sana hasa mkoani Kilimanjaro kutokana na manyoa yao na nyama pia.

MAADUI NA CHANGAMOTO KWA PIMBI WA MIAMBA

Maadui wakuu wa wanyama hawa ni Simba, Chui, Fisi, Mbweha, ndege kama Tai, na nyoka hasa Chatu wa kwenye miamba.

Mpaka sasa bado hakujawa na tishio kwa pimbi hawa. Nadhani ni kwasababu wanapatikana sana maeneo tengefu ya uhifadhi wa wanyamapori hivyo wanakuwa na ulinzi wa kutosha. Japo kwa jamii ya pimbi wa kwenye miti tishio kubwa sana kwao ni uharibifu wa misitu kwani huathiri sana makazi yao.

MUHIMU…Napenda nikudokezee kidogo umuhimu mkubwa sana wa wanyama hawa, baadhi ya tafiti zinaonesha kuwa mkojo na kinyesi cha pimbi ni dawa kubwa sana ya ugonjwa wa KIFAFA. Pili nikwamba pimbi wana uwezo wa kula majani ambayo ni sumu kwa wanyama wengine hivyo husaidia kupunguza athari kwa wanyama ambao wangeweza kula majani haya na kufa kitu ambacho ni hasara kubwa sana kwa taifa na uchumi wetu kiujumla. Hebu fikiria wanakufa tembo au faru kwa kula majani ya sumu endapo tungekuwa hatuna pimbi kwenye maeneo ya hifadhi za wanyamapori.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages