Mambo ni motoooo!! Mpiga picha maarufu hapa bongo Andrew Kisula a.k a Kifesi hii leo ametangaza kuacha kazi kama mpiga picha wa Diamond Platinumz. Kifesi amechukua uamuzi huo ikiwa ni siku chache tangu Chibu kuachana na Zari theboss Lady.
Akiongea na #mukamafunny blog kwa njia ya simu Kifesi amedai kwamba sababu alizoziandika katika ukurasa wake wa Instagram ndo hizo hizo na hana zaidi ya hapo na akadai kwamba hajaachana na Diamond kwa ugomvi bali ni kwa nia njema.
Alipoulizwa kama kitendo cha Mondi kutemana na Zari kimechangia yeye kuacha kupiga picha kwa Simba wa Tandale, Kifesi amejibu kwamba hamna kitu kama hicho.
Ikumbukwe kwamba kipindi Diamond ametengana na Zari kwa mara ya kwanza, Kifesi alitumia muda wake mwingi kumsihi Diamond arejeshe amani katika familia yake hiyo sasa mara hii ya pili ndo ameonekana kuwa kimya katika hilo na hii leo amechukua uamuzi wa namna hiyo.
Aidha Kifesi amedai kwamba ameacha kufanya kazi na Diamond ili aweze kumrudia Mungu ikiwa ni pamoja na kujiajiri mwenyewe katika miradi yake.
No comments:
Post a Comment