ROMA ATIMIZA VIGEZO VYA BASATA, AFUTA RASMI WIMBO WA KIBAMIA - MUKAMAFUNNY BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 5, 2018

ROMA ATIMIZA VIGEZO VYA BASATA, AFUTA RASMI WIMBO WA KIBAMIA

Rapa Roma Mkatoliki, akikabidhiwa cheti cha usajili kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata

Rapa Roma Mkatoliki, akikabidhiwa cheti cha usajili kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Godfrey Mungereza, baada ya kupewa masharti ya kufanya hivyo na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

RAPA Roma Mkatoliki, leo Alhamisi amekabidhiwa cheti cha usajili kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) baada ya kupewa masharti ya kufanya hivyo na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo ili aweze kufutiwa adhabu yake ya kutojihusisha na muziki kwa miezi sita.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar, Ibrahim Mussa’ maarufu kwa jina la Roma Mkatoliki aliwashukuru watu wote waliopaza sauti hadi kufutiwa adhabu hiyo, huku akiwaasa wasanii wenzake kuchukua hatua mapema za kujisajili.

Aidha Roma alisema kuwa, kitendo cha wimbo wake wa Kibamia ni sawa huku akivitaka vyombo vya habari kuacha kuupiga wimbo huo.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Godfrey Mungereza (kulia) akizungumza jambo.

,
Rapa Roma Mkatoliki akiwa katika ofisi ya Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).
Chanzo.: globalpublishers

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages